Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 126 2023-09-08

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:-

Je, lini Serikali itafanya mapitio ya bei ya nauli za Shirika la Ndege Tanzania?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kawaida nauli za safari za ndege hupangwa na soko kulingana na aina ya huduma inayotolewa. ATCL kama ilivyo kwa mashirika mengine ya ndege yanayotoa huduma zake kibiashara, nauli zake zinapangwa na soko kwa kuzingatia matakwa ya sheria za ushindani ambapo vigezo vinavyotumika katika kupanga nauli hizo ni pamoja na gharama za uendeshaji ili kuhakikisha kuwa mashirika ya ndege yanahimili ushindani wa soko na kujiendesha kwa tija na ufanisi.