Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 69 2023-09-04

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanzisha Mamlaka ya Kuratibu na Kupambana na Magonjwa Yasiyoambukiza?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Afya imekwishaunda programu maalum ya kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza ndani ya Idara ya Tiba ambayo ina jukumu la kuandaa miongozo na mikakati ya kisekta kwenye mapambano dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Waziri Mkuu imekwishatekeleza jukumu hili kwa kukiongezea jukumu Kitengo cha Afya Moja (One Health) kusimamia magonjwa yasiyoambukiza chini ya Kurugenzi ya Menejimenti ya Maafa, naomba kuwasilisha.