Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 58 2023-09-04

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu kwa kiwango cha lami?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing'oma Mabula, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu ina urefu wa kilometa 10.5. Serikali imekamilisha usanifu kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami ambapo kiasi cha shilingi bilioni 20 zinahitajika. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali ilitenga shilingi billioni 5.36 kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya urefu wa kilometa 5.04 kiwango cha lami; kilometa 1.725 kiwango cha zege; kilometa 1.8 kiwango cha changarawe; na kilometa 0.7 kiwango cha mawe.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imetenga shilingi bilioni 3.42 kwa ajili ya ujenzi wa barabara kilometa 2.2 kiwango cha lami; kilometa 1.0 kiwango cha zege; kilometa 6.29 kwa kiwango cha changarawe; na kilometa 2.0 kiwango cha mawe.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuweka kwenye mpango Barabara ya Mkuyuni hadi Mahandu na barabara nyingine katika Jimbo la Nyamagana kwa kutenga bajeti kwa ajili wa ujenzi na matengenezo ya barabara hizo, ahsante. (Makofi)