Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 27 2023-08-30

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -

Je, Serikali haioni kuwa kufutwa kwa Form 2c katika huduma ya Bima ya Afya inakosesha mgonjwa kupata dawa iliyokosekana hospitali aliyotibiwa?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT FESTO J. DUGANGE) K.n.y. WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Nkenge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, maamuzi ya Serikali ya kusitisha matumizi ya fomu za dawa (Form 2C) katika vituo vya kutolea huduma za afya yalifanyika kwa kuzingatia manufaa yake, ikiwemo utekelezaji wa maelekezo ya watoa huduma wote wa Serikali. Kwamba kuwe na utaratibu wa kuanzisha maduka ya dawa yanayomilikiwa na hospitali na hivyo kuongeza mapato ya ndani ya hospitali. Pia kuepusha usumbufu kwa wananchi wa kutafuta dawa nje ya hospitali na hivyo kusabisha lawama zisizo za lazima kwa Serikali. Vilevile na kuepusha vitendo vya udanganyifu vinavyofanywa katika eneo la dawa dhidi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, Wizara imevielekeza vituo vya kutolea huduma kuweka utaratibu wa Mgonjwa kupata dawa iliyokosekana hospitali aliyotibiwa ili kuepusha usumbufu kwa wananchi. Ahsante.