Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 380 2023-05-19

Name

Mohamed Abdulrahman Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN. MWINYI aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga ofisi ya NIDA katika wilaya ya Mkoani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Abdulrahman Mwinyi, Mbunge wa Jimbo la Chambani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza mpango wa ujenzi wa ofisi za usajili za wilaya kwa awamu. Katika awamu ya kwanza Serikali imejenga ofisi 13 na awamu ya pili inatarajia kujenga ofisi 31 kuanzia mwaka wa fedha 2023/2024. Serikali kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa itaendelea kujenga ofisi za usajili kulingana na upatikanaji wa fedha kwa wilaya nyingine nchini ikiwemo Wilaya ya Mkoani, ahsante.