Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 377 2023-05-19

Name

Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. AHMED A. SALUM aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Kata ya Ishololo wilayani Shinyanga utakamilika?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K. n. y WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ahmed Ally Salum, Mbunge wa Jimbo la Solwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Ishololo wenye ukubwa wa hekta 600 ni mojawapo ya miradi ambayo ilikuwa ikitekelezwa kupitia mpango wa kuendeleza kilimo wilayani (District Agricultural Sector Investiment Projects). Kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB). Ufadhili wa mpango huu ulifikia kikomo tarehe 31/12/2013 kabla ya mradi huo kukamilika. Wakati mpango wa utekelezaji wa DASIP unafikia kikomo, Utekelezaji wa Mradi wa Ishololo ulikuwa umefikia aslimia 23.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imepanga kufanya mapitio ya usanifu katika mradi wa Ishololo ili kupata gharama halisi za kukamilisha mradi huo. Ukarabati wa mradi huo utapangwa katika Mwaka wa Fedha 2024/2025.