Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 376 2023-05-19

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO K.n.y. MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inawapa elimu ya utunzaji mazingira wananchi wanaofanya shughuli za kilimo katika vyanzo na njia za mito ili wafanye kilimo bila kuleta athari za mazingira?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha mpango mkakati wa kutoa elimu kwa umma wa miaka mitano na lengo la mpango mkakati huu ni kuhamasisha umma wa Tanzania kuhusu maendeleo endelevu pamoja na uhifadhi wa mazingira. Mkakati huu umehusisha namna ya utoaji elimu kuhusu matumizi ya ardhi ndani ya mita 60 katika maeneo ya vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, licha ya Serikali kuruhusu wananchi kufanya shughuli za kilimo kwa umbali wa mita 60 katika maeneo ya vyanzo vya maji, bado kuna changamoto nyingi za uharibifu mkubwa wa mazingira. Hivyo, naomba nichukue fursa hii kuwaomba viongozi wenzangu wa siasa tutumie uwezo wa kuwashawishi na kuhamasisha jamii zinazofanya shughuli za kiuchumi katika maeneo ya vyanzo vya maji na kuhifadhi mazingira.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.