Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 29 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 374 2023-05-19

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Bajeti ya TARURA inazingatia mitandao ya Barabara katika Halmashauri?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Jimbo la Rungwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu la msingi la TARURA ni kuhakikisha kuwa bajeti inayotengwa inaendana na mtandao wa barabara zilizopo katika Halmashauri nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kendelea kutekeleza jukumu hili, Serikali imekuwa ikiongeza bajeti ya barabara ambapo katika mwaka wa fedha 2020/2021 kiasi cha shilingi milioni 962.48 kilitengwa katika mwaka wa fedha 2023/2024. Kumekuwa na ongezeko la bajeti ambapo shilingi bilioni 2.31 zimetengwa kwa ajili ya kazi za barabara katika Wilaya ya Rungwe.