Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 33 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 433 2023-05-25

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J MTEMVU aliuliza: -

Je, nini mkakati wa kushughulikia malalamiko ya ajira za Kada ya Afya na Elimu kutolewa kwa waombaji wanaotoka baadhi ya maeneo?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa kifungu cha 2.1. 2 cha Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma, Toleo la Pili la mwaka 2008 na Kanuni D.6 ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma za mwaka 2009 ikisomwa kwa pamoja na Kanuni 12(1) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2022, ajira kwa nafasi zilizo wazi katika Utumishi wa Umma hujazwa kwa ushindani wa wazi kwa kufanya usaili na kupata washindi katika nafasi husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niliarifu Bunge lako kuwa, Serikali haitoi ajira kwa kuzingatia maeneo. Waombaji wote wa kazi Serikalini huchukuliwa kuwa na haki sawa na hivyo wote hupimwa na kuchujwa kwa vigezo vinavyofanana bila upendeleo wowote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwahimize Watanzania wote wenye sifa stahiki kutoka maeneo yote nchini wajitokeze kuomba nafasi za kazi pindi zitakapotangazwa na Mamlaka zinazoshughulikia ajira nchini ili waweze kushindana na waombaji wengine.