Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 393 2023-05-22

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, kuna mikakati gani ya kudhibiti mifugo katika Bonde la Ihefu na Mto Kilombero?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Soud Mohammed Jumah, Mbunge wa Jimbo la Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Oktoba, 2022 Serikali kupitia Kamati ya Mawaziri Nane wa Kisekta inayoshughulikia migogoro ya ardhi katika vijiji 975 nchini, ilitoa tamko kuhusu utatuzi wa mgogoro wa mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa Ruaha na baadhi ya vijiji vya Wilaya za Mbarali na Chunya. Ili kudhibiti mifugo katika Bonde la Ihefu na Mto Kilombero, jumla ya vijiji 16 vimeandaa mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji na kutenga maeneo kwa ajili ya malisho ili kuwezesha ufugaji katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kudhibiti mifugo kutoka katika maeneo mengine kwenda kwenye Bonde la Mto Kilombero kutafuta malisho na maji katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali inajenga mabwawa ya maji kwa ajili ya mifugo katika Halmashauri za Morogoro DC Kijiji cha Kongwa na Kibaha DC Kijiji cha Viyenze. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imeanzisha mashamba darasa 100 ya malisho katika Halmashauri 44 zikiwemo Halmashauri zinazopakana na Bonde la Ihefu na Mto Kilombero ili wafugaji waweze kujifunza kuzalisha malisho na hivyo kutulia katika maeneo yao ya ufugaji.