Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 386 2023-05-22

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela ambayo ujenzi wake umesimama?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe Mlaghila Jumbe, Mbunge wa Jimbo la Kyela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Kyela inatekeleza ujenzi wa jengo la ghorofa la kutoa huduma ya mama na mtoto katika hospitali ya wilaya. Utekelezaji wa mradi ulianza Septemba, 2019 chini ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa gharama ya shilingi bilioni 3.81. Aidha, hadi kufikia Aprili, 2023 Serikali imeshatoa shilingi bilioni 2.75 na ujenzi umefikia asilimia 72.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 Serikali imetenga shilingi milioni 800 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi, na Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa mradi huo.