Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 358 2023-05-17

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua zao la kahawa Wilayani Lushoto?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya waziri wa kilimo ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Shaban Omari Shekilindi Mbunge wa Lushoto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanzisha kitalu cha miche ya kahawa katika eneo la Jegestal ili kuwezesha upatikanaji wa miche kwa wakulima wa kahawa Wilayani Lushoto. Hadi kufikia tarehe 15 Mei, 2023 jumla ya miche 227,905 imezalishwa na imeanza kusambazwa kwa wakulima mwezi Mei, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania imekiwezesha Chama Kikuu cha Ushirika cha Usambara kuingia mkataba na Kampuni ya Mambo Coffee Company Ltd na kupata cheti cha kilimo hai (Organic Certification) kitakachowezesha chama hicho kuuza kahawa yake kwenye soko maalum. Hatua hizo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kufufua na kuendeleza kilimo cha zao la kahawa katika Wilaya ya Lushoto.