Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 353 2023-05-17

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: -

Je, kwa nini Halmashauri ya Magharibi “A” imeweka Sheria ya Kodi na VAT kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji, Mbunge wa Mwera, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za Mfuko wa Jimbo hutolewa mujibu wa Sheria ya Mfuko wa Jimbo, Sura 96 ya mwaka 2009. Aidha, fedha hizi zinatumika kwa kuzingatia miongozo, kanuni na taratibu za usimamizi wa fedha za umma. Kila upande wa Serikali zetu mbili una utaratibu wa usimamizi wa matumizi ya fedha za umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itashirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzizar kufuatilia utaratibu unaotumika na Halmashauri ya Magharibi “A” kwenye Mfuko wa Jimbo. Aidha, dhamira ya Serikali ni kuendelea kutoa fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo kwa pande zote mbili kwa ajili ya kuboresha huduma za jamii na kuwaletea wananchi maendeleo.