Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 352 2023-05-17

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Je, ni changamoto gani mpya za Muungano zimejitokeza?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa hakuna changamoto za Muungano zilizojitokeza. Sote tunafahamu kuwa Muungano wetu umeendelea kuimarika ambapo wananchi wa pande zote mbili wameendelea kunufaika kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mafanikio ya kutokuwa na changamoto mpya ni kutokana na jitihada za serikali zetu mbili za Muungano kuweka Muongozo mzuri wa kushughulikia changamoto kwa haraka zinapojitokeza katika hatua za awali. Lengo la Serikali zote mbili ikiwa ni kuhakikisha changamoto zote zinazopitiwa zinapatiwa ufumbuzi na kuendelea kuimarisha Muungano ili kuepusha changamoto mpya kujitokeza, nakushukuru.