Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 350 2023-05-17

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. DEO K. SANGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaowaongezea posho Madiwani?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliongeza posho za Madiwani ambapo mwaka 2012 posho hizo ziliongezwa kutoka shilingi 120,000 hadi shilingi 250,000 kwa mwezi sawa na ongezeko la asilimia 108.3. Aidha, katika mwaka wa fedha 2014/2015, Serikali ilipandisha tena posho za Madiwani kupitia waraka wa mwaka 2014 kutoka shilingi 250,000 hadi shilingi 350,000 kwa mwezi sawa na ongezeko la asilimia 40 na shilingi 400,000 kwa Meya na Mwenyekiti wa Halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuzijengea uwezo Mamlaka za Serikali za Mitaa ili ziweze kubuni na kuimarisha vyanzo vya mapato pamoja na kudhibiti mianya ya upotevu wa fedha kwa kutumia mifumo ya kieletroniki ya kukusanya na kutumia fedha katika kutekeleza miradi ya maendeleo pamoja na matumizi mengineyo.