Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 348 2023-05-17

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: -

Je, lini Serikali itapunguza tatizo la upungufu wa walimu katika Shule za Sekondari Babati Vijijini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshaanza kupunguza tatizo la upungufu wa Walimu u katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati ambapo katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, walimu 50 walipelekwa katika shule zilizopo Babati Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetangaza nafasi 13,390 za ajira kwa walimu ambapo baadhi ya walimu hao watapangiwa katika Shule zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuajiri walimu na kuwapeleka katika shule zote nchini hususan katika maeneo yenye uhitaji kadri ya upatikanaji wa fedha.