Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Water and Irrigation Wizara ya Maji 346 2023-05-16

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: -

Je, lini ahadi ya kupeleka mradi mkubwa wa maji Tunduma utatekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua tatizo la maji linaloukabili Mji wa Tunduma na hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali inakarabati miradi ya Uhuru, Nyerere, Ipito, Tunduma na miundombinu ya maji safi Mjini Tunduma. Ukarabati huo unatarajiwa kukamilika mwezi Disemba, 2023 na kunufaisha wakazi 37,853 katika Mji wa Tunduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2023/2024, Serikali itaanza kutekeleza mradi mkubwa wa maji kupitia chanzo cha Mto Momba na kwa sasa taratibu za kuajiri Mkandarasi zinaendelea. Kukamilika kwa mradi huo kutaondoa tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji katika Mji huo.