Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 26 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 343 2023-05-16

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaondoa Kijiji cha Ngaresero kwenye eneo la Pori Tengefu la Pololeti baada ya kujumuishwa kimakosa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Lekishon Shangai, Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, kama ifuatavyo: -

Mheshiwa Naibu Spika, Kijiji cha Ngaresero hakipo katika Pori la Akiba Pololeti ila kipo Kata ya Ngaresero, Tarafa ya Sale. Kijiji hicho ni mojawapo ya vijiji ambavyo vipo ndani ya Pori Tengefu Ziwa Natron. Kulingana na Sheria ya Ardhi Namba 4 ya mwaka 1999 na marekebisho yake ya mwaka 2019, ardhi ya Pori Tengefu Ziwa Natron ipo kwenye kundi la ardhi ya hifadhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Pori Tengefu Ziwa Natron ni moja kati ya maeneo yaliyotolewa maelekezo na Baraza la Mawaziri kuwa lipandishwe hadhi. Hivyo, wakati wa utekelezaji wa maelekezo hayo, wananchi wa kijiji cha Ngaresero watashirikishwa.