Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 25 Water and Irrigation Wizara ya Maji 331 2023-05-15

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatatua tatizo la ukosefu wa maji katika Jimbo la Mbogwe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nicodemus Henry Maganga Mbunge wa Jimbo la Mbogwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji Wilayani Mbongwe ni wastani wa asilimia 55. Katika kupunguza kero ya maji kwa wananchi wa Wilaya hiyo, Serikali ina mipango ya muda mfupi na muda mrefu, ambapo Katika mpango wa muda mfupi Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji ya Iponya, Kagera, Kanegere na Lugunga-Luhala. Miradi hiyo imeanza kutoa huduma kwa wananchi. Vilevile, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itachimba visima virefu 28 sambamba na kufanya upanuzi wa miradi ya maji ya Lulembela, Kagera, Kanegere na ujenzi wa miradi mipya ya maji katika vijiji vya Kisumo, Nyang’holongo, Ikobe, Ngemo, Bwendamwizo, Isebya, Ushirika, Mlale, Kadoke, na Mpakali. Kukamilika kwa Miradi hiyo kutaongeza huduma ya maji kufikia wastani wa asilimi 75.

Mheshimiwa Spika, mpango wa muda mrefu ni kutekeleza mradi mkubwa wa kutoa maji Ziwa Victoria kwenda Wilaya ya Mbogwe ambapo usanifu wa mradi huo unaendelea na utakamilikaji katika mwaka wa fedha 2023/2024 na ujenzi kuanza.