Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 25 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 329 2023-05-15

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y. MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Soko la Samaki Kilwa Kivinje?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imefanya tathmini ya athari za mazingira na kijamii katika eneo la Kitongoji cha Miramba kilichopo Kilwa Kivinje kwa ajili ya kujenga miundombinu ya kuhifadhia mazao ya uvuvi ya chumba cha ubaridi, vichanja vya kukaushia dagaa na kuweka mtambo wa kuzalisha barafu na wa kukaushia dagaa kwa kutumia umeme.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi inayofadhiliwa na Mfuko wa Kimataifa wa Kuendeleza Kilimo (IFAD) itaweka miundombinu hiyo katika eneo hilo. Aidha, Serikali itaendelea na mpango wa kufanya tathmini ya athari ya mazingira na kijamii kwa ajili ya ujenzi wa soko la samaki katika eneo hilo kulingana na upatikanaji wa fedha.