Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 25 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 328 2023-05-15

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: -

Je, ni lini Serikalii itajenga barabara ya mchepuko ya Mlima Nyoka (Uyole) hadi Uwanja wa Ndege wa Songwe ili kuondoa msongamano na ajali?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo kwenye maandalizi ya kujenga barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma yenye urefu wa kilomita 218 pamoja na barabara ya mchepuo ya Mlima wa Nyoka pale Uyole hadi Uwanja wa Ndege wa Songwe (Uyole – Songwe Bypass) yenye urefu wa kilomita 48.9 kwa utaratibu wa EPC+F. Hadi sasa Mkandarasi amekwishapatikana na mkataba wa ujenzi utakuwa umesainiwa kabla ya mwisho wa mwezi Juni, 2023, ahsante.