Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 25 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 325 2023-05-15

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde ya mpunga ya Mahenge, Goo na Kwamngumi - Korogwe Mjini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alfred James Kimea, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mabonde ya umwagiliaji ya Mahenge, Goo na Kwamngumi ni miongoni mwa maeneo ya uzalishaji wa mpunga katika Halmashauri ya Mji Korogwe. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ilitenga fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde hayo. Mwezi Aprili, 2023 Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ilisaini mkataba wenye jumla ya Shilingi bilioni 1.85 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa miundombinu katika Bonde la Mahenge na Bonde la Goo.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika Mpango na Bajeti ya mwaka 2023/2024 imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kupata gharama halisi ya kuendeleza miundombinu ya umwagiliaji katika Bonde la Kwamngumi.