Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 25 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 324 2023-05-15

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuimarisha ukusanyaji mapato kwa biashara zinazofanyika mtandaoni?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Judith Salvio Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato, Serikali kupitia Sheria ya Fedha ya Mwaka 2022 ilifanya marekebisho ya Sheria ya Kodi ya Mapato, Sura Na.
332 na Sheria ya Ongezeko la Thamani, Sura Na. 148 ili kuwezesha kutoza kodi kwenye biashara zinazofanyika kwa njia ya mtandao. Aidha, Mamlaka ya Mapato Tanzania imeanzisha kitengo maalum kinachosimamia biashara za mtandao, ikiwa ni pamoja na kubuni na kuboresha mifumo ya usimamizi wa biashara za mtandao ili kuwezesha utambuzi, usajili na ukusanyaji wa kodi stahiki.

Mheshimiwa Spika, mikakati mingine ni pamoja na kuwajengea uwezo Maafisa wa Kodi juu ya namna ya kutathmini na kukusanya mapato ya kodi yanayotokana na biashara za mtandao, ahsante.