Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 25 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 322 2023-05-15

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha huduma za dialysis kwa Wagonjwa wenye kipato cha chini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy John Sabu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikitoa huduma za matibabu ikiwemo huduma ya kusafisha figo (dialysis) kwa wagonjwa wote bila kujali kipato cha mgonjwa husika. Huduma hizi kwa sasa zinatolewa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Hospitali za Rufaa za Kanda, Mikoa na Hospitali Maalum, ikiwemo Hospitali ya Chuo Kikuu cha Dodoma.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa wito kwa wananchi wenye kipato kidogo kufuata taratibu zinazopelekea wao kupata misamaha ya huduma ikiwemo huduma hii ya usafishaji wa figo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.