Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 25 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 319 2023-05-15

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kutoka Iyula – Ipyana hadi Idunda – Vwawa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Jimbo la Vwawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali ilitenga shilingi milioni 250 kwa ajili ya kufanya matengenezo ya barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 10 kwa kiwango cha changarawe. Katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, Serikali imechonga kipande cha barabara hiyo chenye urefu wa kilometa 3.5 kilichobakia kutoka Idunda kwenda Kitongoji cha Itete kilichopo mpakani mwa Wilaya ya Songwe na Mbeya kwa shilingi milioni 10.5.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuweka mipango ya matengenezo ya barabara hii kulingana na upatikanaji wa fedha.