Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 25 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 318 2023-05-15

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY K.n.y. MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa maabara za sayansi katika shule za sekondari utakamilika kama ilivyokusudiwa katika bajeti ya 2022/2023?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilitoa kiasi cha shilingi milioni 180 kwa ajili ya ukamilishaji wa maabara Sita Halmashauri ya Mji wa Mbulu na tayari mabara hizo zinatumika.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ilitenga na kutoa shilingi milioni 30 kupitia mapato ya ndani ili kukamilisha ujenzi wa vyumba viwili vya maabara na ujenzi huo upo katika hatua ya umaliziaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga na kupeleka fedha kwa ajili ya umalizaji wa maabara 11 ambazo hazijakamilika kadri ya bajeti itakavyoruhusu.