Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 301 2023-05-11

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha kila Kata inakuwa na Mahakama hasa maeneo ya Vijijini?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria napenda sasa kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inayo azma na dhamira ya kusogeza huduma za haki karibu na wananchi, hususan kwa kujenga na kukarabati majengo ya Mahakama. Katika kutekeleza azma hii, tunao mpango wa ujenzi na ukarabati wa majengo ya Mahakama, katika ngazi zote, kuanzia Mahakama za Mwanzo hadi Mahakama za Rufani.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Mahakama za mwanzo, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kuwa walau kila Tarafa inakuwa na Mahakama ya Mwanzo na baadaye tuweze kwenda hadi ngazi ya Kata kadri upatikanaji wa fedha utakavyoruhusu. Ahsante.