Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 271 2023-05-09

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga nyumba za Askari Polisi katika Kituo cha Wilaya ya Micheweni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua mahitaji ya nyumba za makazi ya kuishi askari Polisi katika Wilaya ya Micheweni. Mpaka sasa ujenzi unaoendelea ni wa hanga la kuishi familia 18 za askari na uko kwenye hatua za umaliziaji. Kiasi cha shilingi milioni 60,000,000 kinahitajika ili kumalizia na fedha hizo zinatarajiwa kuombwa kutoka Mfuko wa Tuzo na Tozo kwa mwaka wa fedha 2023/2024. Serikali itaendelea kujenga nyumba za maofisa na askari kutegemea upatikanaji wa fedha, ahsante.