Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Water and Irrigation Wizara ya Maji 263 2023-05-08

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, ni lini changamoto ya maji ndani ya Jimbo la Momba litatatuliwa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe Mbunge wa Jimbo la Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua adha ya maji wanayopata Wananchi wa Wilaya ya Momba na tayari hatua zimeanza kuchukuliwa. Katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 miradi ya maji ya Msangano-Naming’ongo, Isanga - Kakozi na Tindingoma - Mlomba inaendelea kutekelezwa na itahudumia vijiji 11 vya Msangano, Nkala, Makamba, Naming'ongo, Yala, Ipata, Ntinga, Chindi, Isanga, Kakozi na Mlomba.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maji kupitia chanzo cha maji cha Mto Momba ili kuhakikisha wananchi katika vijiji vilivyobaki Wilayani Momba wanapata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza.