Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 258 2023-05-08

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya kutoka Geita – Bukoli hadi Kahama?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tumaini Bryceson Magessa, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imepata fedha kiasi cha dola za Marekani milioni 40 sawa na shilingi bilioni 92 kupitia Mkataba wa makubaliano na Kampuni ya Kuchimba Madini ya Barrick kwa ajili ya ujenzi wa kipande cha barabara kutoka Kahama – Bulyanhulu hadi Kakola urefu wa kilometa 73. Kwa sasa kazi ya kupitia usanifu inafanyika kwa pamoja kati ya wataalam wa Serikali na Kampuni ya Barrick. Kazi zimepangwa kutangazwa kabla ya mwisho wa mwezi Juni, 2023 na ujenzi unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha wa 2023/2024.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali itatenga fedha katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kipande kilichobaki cha barabara kutoka Geita – Bukoli – Bulyanhulu Junction kilometa 57.4, ahsante.