Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 257 2023-05-08

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: -

Je, lini Serikali itaimarisha ulinzi na usalama wa maeneo ya maziwa na bahari ili kulinda rasilimali pamoja na wavuvi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi ina wajibu wa kulinda maisha na mali za wananchi wake. Katika Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2023/2024, tumepanga kutenga shilingi billioni 4.5 kwa ajili ya kununulia Boti 10 za doria zitakazotumika kwenye maeneo ya bahari na maziwa. Pindi boti hizo zitakapofika zitagawiwa maeneo yenye changamoto kubwa za uhalifu wa majini likiwemo eneo ya Rorya.