Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 256 2023-05-08

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaongeza nyumba za makazi kwa Askari Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asya Sharif Omar, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imekamilisha ujenzi wa nyumba moja ya kuishi familia nne za askari katika eneo la Finya, Wilaya ya Wete. Mradi unaoendelea sasa ni ujenzi wa hanga la kuishi familia 18 za askari kwenye Kituo cha Polisi Micheweni. Ujenzi huo umefikia hatua ya kumalizia.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imepanga kutumia kiasi cha Sh.270,121,580 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba mbili za kuishi familia nne za askari Polisi eneo la Konde Wilaya ya Micheweni. Utaratibu wa kujenga nyumba za makazi ya askari ni endelevu na utakuwa ukifanyika kwa kadri ya upatikanaji wa fedha, ahsante.