Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 255 2023-05-08

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Tanganyika?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimwa Moshi Seleman Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi Wilaya ya Tanganyika, Mkoa wa Katavi limepatiwa eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 85,229 na Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi daraja B, pamoja na nyumba za makazi ya askari katika eneo la Majalila. Ujenzi wa kituo hicho uko kwenye hatua ya msingi na unashirikisha nguvu za wananchi na wadau akiwemo Mheshimiwa Mbunge. Upimaji wa eneo umeshafanyika na kiasi cha fedha shilingi 20.225 kinahitajika kama gharama za ardhi na maombi yameshatumwa Makao Makuu ya Polisi kwa ajili ya kulipa kwenye halmashauri ya wilaya, ili kupata hati miliki itakayowezesha Wizara kutenga fedha za ujenzi wa kituo na nyumba za makazi ya askari kwenye bajeti ya Serikali katika kuunga mkono jitihada za wananchi na wadau, nashukuru.