Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 253 2023-05-08

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti mafuriko ambayo husababisha uchafuzi wa mazingira na kuongeza umaskini katika Jimbo la Mwera?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji, Mbunge wa Jimbo la Mwera kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kudhibiti kutokea kwa mafuriko katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Magharibi A yakiwemo maeneo ya Jimbo la Mwera, hatua zilizochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni pamoja na hatua zifuatazo: -

(i) Kuunda Kamati ya Kukabiliana na Maafa ya Wilaya ya Magharibi A yenye jukumu kuu la kuratibu utekelezaji wa Mpango wa Wilaya wa Kukabiliana na Maafa wa mwaka 2022; sambamba na kuwaelimisha wananchi.

(ii) Kuandaa mpango wa wilaya wa kukabiliana na maafa ambao umeainisha wadau, majukumu yao na mpango wa utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais itaendelea kufanya tathmini ya kina katika maeneo yote yanayokumbwa na mafuriko nchini ikiwemo maeneo ya Jimbo la Mwera.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.