Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 251 2023-05-08

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Mto Duma Bariadi Mkoani Simiyu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mto Duma ni mto mkubwa unaoanzia Kata za Gibishi kupitia Kata ya Matongo, Mwaubingi na Gilya. Mto huu ni wa msimu ambao hujaa kipindi cha Mvua kutokea Mbuga ya hifadhi ya Serengeti kuelekea Ziwa Victoria na hukauka kipindi cha kiangazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kukidhi haja ya kuwa na mawasiliano kwa Wananchi wanaotenganishwa na mto huu, jumla ya madaraja mawili yanahitajika ambapo hadi sasa ni daraja moja limejengwa katika barabara ya Igegu – Matongo - Gibishi. Kwa upande wa barabara ya Gasuma – Gilya, Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 50 katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa daraja ili kujua gharama halisi za ujenzi wake.