Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 250 2023-05-08

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafunga taa za barabarani eneo la Tunduru Mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Tunduru ina mtandao wa barabara wenye urefu wa kilometa 1,200. Kati ya hizo, barabara za tabaka la lami ni kilometa 4.5, barabara zenye tabaka la changarawe ni kilometa 285 na barabara za tabaka la udongo ni kilometa 914.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali kupitia TARURA ilifunga taa za barabarani 16 kwa gharama ya shilingi milioni 72 katika barabara ya Bus Stand –Sinabei Guest House, TUDECO – Tunduru Sekondari – Borrow Pit, NMB – Ushirika na Nguzo Sita – Muungano – Camp David. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya taa 20 za barabarani zitafungwa kwa gharama ya shilingi milioni 90 katika barabara ya Isalmic Centre – Amazon – Mkunguni na Bus Stand – Mseto – Mkunguni baada ya kukamilishwa kwa ujenzi wa barabara. Mwaka wa fedha 2023/2024 TARURA imetenga shilingi milioni 270 kwa ajili ya kufunga taa 60.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini itaendelea kuhudumia miundombinu ya barabara ya Mji wa Tunduru kwa kuweka katika mipango yake ujenzi na matengenezo ya barabara ikiwemo ufungaji wa taa za barabarani kulingana na upatikanaji wa fedha.