Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 249 2023-05-05

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga malambo ya kunyweshea mifugo katika Kata ya Chala, Kate, Myula na Nkandasi Wilayani Nkasi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto ya upungufu wa maji kwa ajili ya mifugo katika Kata za Chala, Kate, Myula na Nkandasi, Serikali katika mwaka wa fedha 2023/2024, imepanga kufanya tathmini ya miundombinu ya maji na usanifu utakaowezesha kujenga malambo au kuchimba visima virefu katika maeneo hayo. Matokeo ya tathmini hiyo yataiwezesha Serikali kujenga miundombinu hiyo kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, kutokana na kuongezeka kwa changamoto ya uhaba wa maji kwa ajili ya mifugo, nazikumbusha Halmashauri za Wilaya nchini kutekeleza Waraka wa Rais Na.1 wa mwaka 2002 kuhusu kutenga asilimia 15 ya mapato yatokanayo na Sekta ya Mifugo ili kujenga na kukarabati miundombinu ya maji. Pia, nitoe wito kwa wafugaji na wadau wengine kuwekeza kwenye ujenzi wa malambo au kuchimbaji visima virefu.