Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 247 2023-05-05

Name

Ameir Abdalla Ameir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. AMEIR ABDALLAH AMEIR aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuhakikisha utalii wa ndani unaimarika?

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utaii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ameir Abdallah Ameir, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika; katika kuhakikisha utalii wa ndani unaendelea kuimarika nchini, Wizara inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kukuza utalii wa ndani ikiwemo: -

i. Kuwa na huduma bora zenye gharama nafuu kwenye vivutio zikiwemo malazi, chakula, usafiri na viingilio;

ii. Kuendelea kuhamasisha makundi mbalimbali ya kijamii ikiwa ni pamoja na wanafunzi, wajasiriamali, wafanyakazi na makundi maalum kutembelea maeneo ya vivutio vya utalii na pia kufanya mikutano; na

iii. Kuendelea kutoa elimu kwa umma na kutumia chaneli maalum (Tanzania Safari Channel) ya kutangaza utalii kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii pamoja na kuhamasisha wananchi kutembelea vivutio hivyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuongeza maeneo ya utalii, kuibua vivutio na mazao mapya ya utalii na kuendeleza miundombinu ya utalii katika kanda zote za utalii nchini.