Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 238 2023-05-05

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka Watumishi pamoja na Vifaa Tiba katika Hospitali ya Halmashauri ya Ushetu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Peter Cherehani, Mbunge wa Jimbo la Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuajiri watumishi wa kada za afya. Katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 na 2021/2022, watumishi wa kada hiyo 10,462 waliajiriwa kote nchini. Katika ajira hizo, Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu ilipangiwa watumishi 55 na watumishi 25 walipelekwa kwenye Hospitali ya Halmashuri ya Wilaya ya Ushetu. Aidha, Aprili, 2023, Serikali imetangaza nafasi 8,070 za ajira kwa kada za afya ambapo baadhi ya watumishi hao watapelekwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Ushetu.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2020/2021, Hospitali ya Wilaya ya Ushetu ilipelekewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kupitia Bohari Kuu ya Dawa (MSD) na tayari MSD wameanza kusambaza vifaa tiba kwenye Hospitali za Halmashauri 67 ikiwemo Hospitali ya Wilaya ya Ushetu. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, Hospitali hiyo imepokea shilingi milioni 100 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya macho na meno. Vilevile, Hospitali hii imepokea vifaa tiba kwa ajili ya jengo la Kutolea Huduma za Dharura (EMD).