Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 237 2023-05-05

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaboresha miundombinu ya Shule za Mtapa, Kanani na Wangutwa Wilayani Wanging’ombe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2020/2021, kupitia mapato ya ndani, Halmashauri ya Wilaya ya Wanging`ombe ilipeleka shilingi milioni mbili kwa Shule ya Msingi Kanani kwa ajili ya ujenzi wa vyoo. Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali ilitoa shilingi milioni 10 kwa ajili ya ukamilishaji wa vyumba vya madarasa. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali imetenga shilingi milioni 75 kwa ajili ya ukarabati katika shule hiyo.

Mheshimiwa Spika, Shule ya Msingi Wangutwa inaendelea kufanyiwa ukarabati kwa kushirikiana na wananchi. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 Serikali ilipeleka shilingi milioni 61.6 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa matundu ya vyoo. Vilevile, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, shule hiyo imetengewa shilingi milioni 75 kwa ajili ya kuongeza madarasa matatu.

Mheshimiwa Spika, vilevile, katika mwaka wa fedha wa 2019/2020, Serikali ilitoa shilingi milioni 12.5 kwa ajili ya ukamilishaji wa vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Msingi Mtapa. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 shule hiyo ilipelekewa shilingi milioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa.