Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 18 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 234 2023-05-04

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani kupitia TBA kuwajengea nyumba watumishi wa Serikali ya Muungano kwa upande wa Zanzibar?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Usonge Hamad, Mbunge wa Chaani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeanzishwa chini ya Sheria ya Wakala, Sura 245 ikisomwa pamoja na Agizo la Uanzishwaji wa Wakala GN. Na. 24 la tarehe 14 Februari, 2003. Moja ya jukumu la msingi la TBA ni kujenga na kukarabati nyumba na majengo ya Serikali kwa ajili ya makazi kwa watumishi wa umma Tanzania Bara.

Mheshimiwa Spika, Jukumu la ujenzi wa nyumba kwa watumishi wa Umma kwa upande wa Zanzibar liko chini ya Wakala wa Majengo Zanzibar (ZBA). Hata hivyo, TBA na ZBA wanashirikiana na kushauriana kwenye mambo mbalimbali ya kitaalam na kujengeana uwezo, ahsante.