Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 18 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 231 2023-05-04

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, lini Jeshi la Uhifadhi litapata Kamishna Jenerali na kuleta muunganiko katika divisheni za NCAA, TANAPA, TAWA na TFS?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Uhifadhi Wanyamapori na Misitu (The Wildlife and Forest Conservation Service) lilianzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 10(1) cha Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori Sura ya 283.

Mheshimiwa Spika, utendaji wa taasisi zinazounda Jeshi hilo upo chini ya Kamishna wa Uhifadhi wa kila taasisi nao watakuwa ndio makamanda wa taasisi zao. Muundo wa Jeshi la Uhifadhi unaotumika kwa sasa unafanya kazi vizuri. Endapo kutabainika kuwa na changamoto katika kutekeleza mfumo huo, Serikali itafanya marejeo ya Sheria ya

Wanyamapori ili kuwezesha kuwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhifadhi Wanyamapori na Misitu.