Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 18 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 230 2023-05-04

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH M. MASSABURI aliuiliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kupeleka Maofisa Usalama Barabarani Falme za Kiarabu na Vietnam ili kujifunza jinsi ya kudhibiti ajali?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Maurice Massaburi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inao utaratibu wa kutoa mafunzo mbalimbali kwa maofisa wa polisi wa usalama barabarani ndani ya nchi na pia kuwapeleka nje ya nchi kujifunza namna bora ya kusimamia na kudhibiti ajali za barabarani.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia mwaka 2015 hadi 2023 Serikali imeshawapeleka maofisa wa usalama barabarani 30 kwenye nchi 15 ambazo ni Marekani, Ujerumani, Japan, China, India, Vietnam, Australia, Switzerland, Falme za Kiarabu, Israel, Tunisia, Misri, Ghana, Rwanda na Afrika Kusini ili kujifunza masuala ya usalama barabarani. Mashirika ya kimataifa na wadau kama JICA, UKAID, WFP, WHO, LATRA, TIRA, TRA, NIT na Baraza la Taifa la Usalama Barabarani wanaendelea kufadhili na kutoa mafunzo juu ya udhibiti na usimamizi wa taratibu za usalama barabarani ili kupunguza ajali nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutoa nafasi za mafunzo ndani na nje ya nchi kwa maofisa wa usalama barabarani ili kupata ujuzi juu ya usimamizi na udhibiti wa ajali kama alivyoshauri Mheshimiwa Mbunge, nashukuru.