Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 229 2023-05-04

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Km 10 kwa kiwango cha lami Mjini Tunduma?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli mwaka 2020 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliahidi ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 10 kwenye Mji wa Tunduma.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa ahadi hiyo umeanza ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya kilometa 2.8 zilijengwa kwa kiwango cha lami na shilingi bilioni 1.39 zilitumika. Aidha, mwaka wa fedha wa 2022/2023 shilingi bilioni 2.3 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa kilomita 3.7 kwa kiwango cha lami ambapo shilingi bilioni 1.64 zimepokelewa na ujenzi umefikia asilimia 45.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kukamilisha ahadi hiyo kadiri ya upatikanaji wa fedha.