Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 228 2023-05-04

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabweni kwenye shule za wasichana wanaosoma masomo ya sayansi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Paulina Daniel Nahato, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutoa kipaumbele katika ujenzi wa mabweni ya wanafunzi katika shule za bweni. Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 Serikali imetoa Shilingi bilioni 30 kwa ajili ya ujenzi wa shule 10 maalumu za sekondari za wasichana za masomo ya sayansi kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita. Ujenzi huu ni awamu ya kwanza ya ujenzi wa shule 26 ambazo kila Mkoa utajengewa shule moja kupitia mradi wa SEQUIP.

Mheshimiwa Spika, mradi huo unahusisha ujenzi wa mabweni tisa katika kila shule na kila bweni litakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 120. Aidha, kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Sekta ya Elimu, Serikali itaendelea kujenga na kukarabati mabweni ili kuongeza nafasi zaidi za wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Sita.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka kipaumbele cha ujenzi wa mabweni kwa shule za kidato cha tano na sita na kwa wanafunzi wote wa kike na wakiume, kwa kuwa wanafunzi wote wana changamoto.