Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 226 2023-05-04

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Chikola na Makanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilipokea vipaumbele vya ujenzi wa vituo vya afya katika Kata za Sanza, Chikola na Makanda zilizopo katika Jimbo la Manyoni Mashariki. Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali ilipeleka Shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kimkakati cha Sanza ambapo ujenzi wa awamu ya kwanza kwa OPD na maabara umekamilika. Ujenzi wa awamu ya pili, unaohusisha wodi ya wazazi, chumba cha upasuaji na laundry upo kati hatua ya ukamilishaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya vya kimkakati nchini ikiwa ni pamoja na kwenye Kata za Chikola na Makanda kadri fedha zitakavyopatikana.