Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 197 2023-04-28

Name

Salim Mussa Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gando

Primary Question

MHE. KASSIM HASSAN HAJI K.n.y. MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuandaa Filamu zenye kueleza Historia ya Nchi?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Salim Mussa Omar, Mbunge wa Gando, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Bodi ya Filamu Tanzania kwa kushirikiana na wadau imewezesha uzalishaji wa filamu zinazohifadhi na kuelezea historia ya nchi yetu.

Mfano Makala ya Uzalendo iliyoandaliwa na Bodi ya Filamu mwaka 2021 kupitia muandaaji filamu Bwana Adam Juma inaelezea historia ya viongozi wetu na ushujaa wao katika kuipambania nchi. Pia, mwaka 2022 Bodi kupitia Studio za Wanene iliandaa makala inayotangaza mandhari ya kupiga picha za filamu na kuelezea maeneo ya kihistoria yaliyopo nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Bodi ya Filamu inaendelea na maandalizi ya filamu inayohusu maisha ya Chifu Mkwawa iitwayo Mkwavinyika. Pia kwa kushirikiana na wadau wa filamu, Bodi inaratibu mpango mahsusi wa uandaaji wa filamu zinazohusu maisha ya viongozi wetu, ambapo itaanza na filamu ya Bibi Titi Mohammed, ikifuatiwa na ya Chifu Kingalu, Mtemi Mirambo pamoja na Mwalimu Nyerere.