Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 196 2023-04-28

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kusaidia kuongezeka kwa bei ya zao la chai kwa wakulima nchini?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bei ya zao la chai hutegemea mwenendo wa Soko la Dunia, soko la ndani na ubora wa chai sokoni. Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali kuhakikisha uwepo wa mazingira bora yanayoleta ushindani ili kuchochea bei ya chai. Katika hatua ya awali, kwa mwaka 2023 bei ya chai imeongezeka kutoka shilingi 312 hadi shilingi 366 kwa kilo. Aidha, mikakati mingine ya kupandisha bei ni kuongeza uzalishaji wa miche bora ya chai, kuendelea kuhamasisha matumizi ya chai nchini, kuanzisha mnada wa chai, kutoa ruzuku ya mbolea na miche bora ya chai ili kuongeza tija na uzalishaji na kuandaa mwongozo wa ubora wa majani mabichi ya chai na kuanzisha kiwanda cha kusindika chai maalumu.