Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 195 2023-04-28

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: -

Je, Serikali haioni ni busara kuuza nyumba kwa Wapangaji wa kota za Ukonga kwa kuwa wameishi miaka mingi bila kufanyiwa ukarabati?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeweka mpango mahsusi wa kukarabati na kuendeleza maeneo yote ya kota nchini ambazo ni nyumba zilizorejeshwa TBA kutoka TAMISEMI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika mwaka huu wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imeanza kukarabati nyumba za kota za Ukonga ambapo kwa sasa TBA imekarabati maghorofa mawili yenye uwezo wa kubeba familia Nane. Ukarabati umehusisha maeneo ya paa, dari, mfumo wa umeme, mfumo wa majisafi na majitaka na upakaji wa rangi, ahsante.