Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 194 2023-04-28

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja litakalounganisha Tanzania Bara na Zanzibar?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazungumzo kuhusu ujenzi wa daraja litakalounganisha Tanzania Bara na Zanzibar yalishaanza kwa kuzihusisha Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, sekta ya ujenzi kwa upande wa Tanzania Bara na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kwa upande wa Zanzibar, ambapo mnamo tarehe 11 Machi, 2023 kwa pamoja walikutana na Wawekezaji Kampuni ya China Overseas Engineering Group Company waliokuwa wameonesha nia ya kujenga daraja hilo. Yatokanayo na kikao hicho bado yanafanyiwa kazi kwa pande zote mbili Tanzania Bara na Zanzibar, ahsante.